Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Issa Machibya, akimkaribisha ofisini kwake Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez, aliyefuatana na Mwakilishi wa UNFPA, Natalia Kanem.
Mratibu Mkazi wa UN hapa nchini Alvaro Rodriguez, akiwaongoza viongozi wengine akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, kuinua mabango yenye jumbe mbali mbali yakiwemo ya kupinga umasikini na kuhimiza elimu bora.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma,Issa Machibya, katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa UN, hapa nchini, Alvaro Rodriguez na Mwakilishi wa UNFPA, Dr. Natalia Kanem, nje ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
Mratibu Mkazi wa UN, Alvaro Rodriguez, akiangalia namna ya utengenezaji wa sabuni alipotembelea kikundi cha wajasiriamali eneo la Katubuka mjini Kigoma.