Jukwaa Huru Mkoa wa Kigoma watoa tamko kuhusu Baraza la Mawaziri


Mwenyekiti wa Jukwaa Huru Mkoa wa Kigoma, Monalisa Joseph Ndala, akiwa na Katibu wa Jukwaa Huru Taifa Mtela

Mwenyekiti wa Jukwaa Huru Mkoa wa Kigoma, Monalisa Joseph Ndala, akiwa na Katibu wa Jukwaa Huru Taifa Mtela Mwampamba.

 

 

Ndugu Wanahabari

Poleni na majukumu ya kuelimisha na Kuhabarisha Taifa hili.
Tulio mbele yenu ni Viongozi wa Jukwaa Huru la Wazalendo kutoka Mkoa wa Kigoma.

Ndugu wanahabari

Sisi Wana Jukwaa Huru la Wazalendo tumekuwa tukifanya matamko mbali mbali katika mikoa tofauti tofauti hapa Nchini.Tumekuwa tukifanya hivi kwa lengo la Kuunga mkono Hotuba ya Mh.Rais Wa Jamhuri ya Muungano waTanzania alioitoa siku akifungua Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Continue reading

By KigomaLive Posted in Habari

Waziri wa Magufuli aianza vibaya “Hapa ni Kazi tu”


Eng. Stella Manyanya, akila kiapo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Eng. Stella Manyanya, akila kiapo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

 

Naibu Waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, amemuomba radhi Rais Magufuli na watanzania wote kwa ujumla kwa kitendo chake cha kukumbwa na kigugumizi na kusita sita muda wote wa kula kiapo na kushangaza wengi waliofuatilia tukio la wakati Rais Magufuli kuwaapisha mawaziri hii leo Jijini Dar es Salaam. Continue reading

By KigomaLive Posted in Habari

Klabu ya Soka yawanunulia Wachezaji wake Boda Boda


Mamlaka ya mapato nchini Uganda (URA) kupitia
timu yake ya URA FC imewapa wachezaji wake
zawadi ya pikipiki maarufu kama ‘bodaboda’
kwa ajili ya kuongeza vipato vyao mbali na
mshara wanaoupata kila mwezi kutoka kwenye
klabu yao.

URA imewasaidi wachezaji wake kwa kuwapa
pikipiki hizo za biashara ‘bodaboda’ ambazo
zimesambaa nchini Uganda na Afrika Mashariki
kwa ujumla kwa ajili ya kusafirisha abiria
pamoja na mizigo.

Kutokana na hali ya maisha kupanda kwenye mji
kuu wa Uganda Kampala, mwenyekiti wa klabu
hiyo Ali Ssekatawa amesema kwamba, hawataki
wachezaji wao wategemee mishahara pekee
hivyo wakaona ni vyema kuwatafutia vyanzo
vingine vya kupata pesa vitakavyowasaidia
kujipatia kipato mbali na kazi yao ya kucheza
mpira.

“Tunaangalia mfumo wa kuwafanya waweze
kujitegemea wenyewe na tukifanikiwa katika hilo
basi wachezaji wetu watacheza vizuri”, amesema
Ssekatawa.

URA ni moja kati ya vilabu maarufu kwenye Ligi
ya Uganda (Uganda Premier League) na
wamekuwa wakiwakilisha ukanda wa Afrika
Mashariki kwenye michuano ya CAF Champions
League pamoja na ile ya Confederation Cup
ambayo kwa pamoja ni michuano mikuwa barani
Afrika kwa ngazi ya vilabu.

Mapema mwaka huu commissioner wa URA FC
Doris Akol aliahidi watawasaidia wachezaji
kujipatia kipato cha ziada na mwenyekiti wa
klabu Ssekatawa amekabidhi bodaboda 17 kwa
wachezaji kwenye uwanja wa mazoezi.

By KigomaLive Posted in Habari

Olunga wa Gor Mahia mchezaji bora Kenya 2015


Mshambuliaji wa Gor Mahia Michael Olunga
ametawazwa kuwa mshindi wa tuzo ya
mwanasoka bora zaidi wa mwaka 2015 nchini
Kenya.

Mshambuliaji huyo wa timu ya Gor Mahia
ametuzwa kombe hilo pamoja na kitita cha
shilingi milioni moja za Kenya au dola elfu kumi
mbali na zawadi nyinginezo kama vile TV kubwa
ya inchi 43.

Sherehe za mwaka huu za kuwatuza wachezaji
bora wa kandanda nchini Kenya zilikuwa za
kipekee kwani mbali na miaka ya nyuma, kitita
kikubwa cha pesa kilitumika kuwapa washindi wa
karibu kila kitengo.

Kulikuwa na jumla ya vitengo 13 vya
kushindaniwa, huku walioibuka washindi
wakipewa pesa taslimu au zawadi chungu nzima
zilizotolewa na kampuni mbalimbali za wafadhili.
Licha ya mwenyekiti wa soka Nchini Kenya Sam
Nyamweya na waziri wa michezo Hassan Wario
wakikwepa kuhudhuria sherehe hizo, zilizofanyika
katika hoteli moja ya kifahari Jijini Nairobi, nyota
wa zamani wa soka nchini Kenya walihudhuria
akiwemo J.J Masiga.

Tuzo ya mwaka huu ya mchezaji bora wa mwaka
lilimwendea chipukizi wa miaka 22 mwanafunzi
wa chuo cha teknolojia cha Kenya na
mshambulizi wa Gor Mahia Michael Olunga.
Tuzo mpya iliyobuniwa mwaka huu ya mchezaji
chipukizi zaidi wa mwaka, ilimuendea George
Mandela wa timu ya Muhoroni FC, kutoka
Magharibi mwa Kenya.

Nayo tuzo ya refa aliyeimarika zaidi mwaka huu,
ilitwaliwa na Raymond Onyango na ile ya naibu
kocha ikatwaliwa na Stephen Deya.
Nayo timu bora zaidi mwaka 2015 ilikuwa
Western Stima baada ya kuzipiku Mathare United
na Sony Sugar.

John Baraza wa timu ya Sofapaka alinyakuwa
tuzo ya mchezaji mwenye nidhamu ya hali ya juu
zaidi mwaka huu.

Ushindani mkali ulishuhudiwa katika tuzo la
maneja bora zaidi wa timu, ambapo hatimaye Bw
Jodali Obondo wa Gor Mahia aliibuka mshindi.
Katika wachezaji, kipa bora mwaka huu wa KPL
alikuwa Bonface Oluoch wa Gor Mahia aliyejipatia
dola elfu tano, huku Farouk Shikalo wa Muhoroni
Youth na Jairus Adira wa wakijipatia dola elfu
mbili kila mmoja.

Mlinzi bora alikuwa mchezaji wa Gor Mahia raia
wa Burundi, Karim Nzigimana.
Tuzo la Kocha bora lilimweendea mkufunzi wa
mabingwa wa ligi kuu nchini Kenya Gor Mahia,
Frank Nutall, ambaye alipewa mkataba huo kwa
misingi kuwa sharti aifanye timu ya Gor kuibuka
mshindi ili apate kazi ya ukufunzi, jambo ambalo
amelitimiza.

By KigomaLive Posted in Habari

Vijana watakiwa kufanya kazi katika Jamii


Mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia UVCCM Mkoa wa Kigoma, Zainab Katimba, akiongea na Vijana wakati akifungua kikao cha Baraza la Vijana.

Mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia UVCCM Mkoa wa Kigoma, Zainab Katimba, akiongea wakati akifungua Kikao cha Baraza la Vijana wa CCM mkoa wa Kigoma.

 

VIJANA wa Chama cha Mapinduzi mkoani Kigoma wametakiwa kushirikiana kwa karibu na watu wa makundi na mahitaji maalum na kujihusisha na shughuli mbali mbali za kijamii ili kujenga imani katika jamii. Continue reading

By KigomaLive Posted in Habari
Image

Picha: Mbunge wa UVCCM Kigoma aongoza Vijana wenzake kufanya usafi


Tazama picha mbali mbali za Mbunge wa Bunge la Jmahuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia UVCCM Mkoa wa Kigoma, Zainab Katimba(aliyevaa Gum Boot), akiwaongoza Vijana wenzake katika zoezi la kufanya usafi, ambapo wamefanya usafi katika eneo la Hospitali ya Maweni.

Tazama picha mbali mbali za Mbunge wa Bunge la Jmahuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia UVCCM Mkoa wa Kigoma, Zainab Katimba, akiwaongoza Vijana wenzake katika zoezi la kufanya usafi, ambapo wamefanya usafi katika eneo la Hospitali ya Maweni.

E80A1866

E80A1815

 

Tazama picha hapa chini Mbunge kupitia UVCCM Mkoa wa Kigoma, Zainab Katimba, alipotembelea Hospitali ya Maweni na Vijana wengine wakiongozwa na Mwenyekiti UVCCM Mkoa wa Kigoma, Peter Msanjila.

Mbunge huyo amewafariji wagonjwa na kutoa zawadi ya sabuni, vinywaji laini na Biskuti, ambapo pia amewapa salaam wagonjwa kutoka kwa Rais John Magufuli, kwamba wawe na matumaini kuhusu huduma za afya.

E80A1749

E80A1727

 

E80A1717

E80A1718

E80A1736

E80A1779

E80A1732

By KigomaLive Posted in Habari

Tazama picha mbali mbali za ziara ya ujumbe wa UN Kigoma


Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Issa Machibya, akimkaribisha ofisini kwake Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez, aliyefuatana na Mwakilishi wa UNFPA, Natalia Kanem.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Issa Machibya, akimkaribisha ofisini kwake Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez, aliyefuatana na Mwakilishi wa UNFPA, Natalia Kanem.

 

Mratibu Mkazi wa UN hapa nchini Alvaro Rodriguez, akiwaongoza viongozi wengine akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, kuinua mabango yenye jumbe mbali mbali yakiwemo ya kupinga umasikini na kuhimiza elimu bora.

Mratibu Mkazi wa UN hapa nchini Alvaro Rodriguez, akiwaongoza viongozi wengine akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, kuinua mabango yenye jumbe mbali mbali yakiwemo ya kupinga umasikini na kuhimiza elimu bora.

 

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma,Issa Machibya, katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa UN, hapa nchini, Alvaro Rodriguez na Mwakilishi wa UNFPA, Dr. Natalia Kanem, nje ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma,Issa Machibya, katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa UN, hapa nchini, Alvaro Rodriguez na Mwakilishi wa UNFPA, Dr. Natalia Kanem, nje ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

 

Mratibu Mkazi wa UN, Alvaro Rodriguez, akiangalia namna ya utengenezaji wa sabuni alipotembelea kikundi cha wajasiriamali eneo la Katubuka mjini Kigoma.

Mratibu Mkazi wa UN, Alvaro Rodriguez, akiangalia namna ya utengenezaji wa sabuni alipotembelea kikundi cha wajasiriamali eneo la Katubuka mjini Kigoma.

E80A1463

 

By KigomaLive Posted in Habari

Kesi ya kupinga matokeo, Kafulila atimiza sharti la Mahakama.


ALIYEKUWA Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, jana alitekeleza agizo la Mahakama Kuu Kanda ya Tabora kwa kutoa Sh. 7,500,000 milioni ili kusikilizwa kwa kesi yake.

Wakati akifungua kesi ya kupinga matokeo ya ubunge yaliyompa ushindi mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hasna Mwilima katika jimbo hilo, mahakama hiyo ilimtaka Kafulila atoe Sh. 15 milioni kama dhamana ya kusikilizwa kesi hiyo yenye washitakiwa watatu.

Kafulila anadai kushinda uchaguzi huo na kwamba, anachohitaji ni kuomba mahakama imvue ubunge Husna na kumtangaza yeye kuwa mshindi.

Awali, Jaji Leila Mgonya anayesikiliza kesi hiyo alimtaka Kafulila kulipa dhamana ya Sh. 5,000,000 kwa kila mshitakiwa na kufanya Sh. 15 milioni kwa washitakiwa watatu.

Kafulila kupitia kwa wakili wake Emmanual Msya, aliwasilisha ombi la kupunguziwa kiasi hicho cha fedha katika mahakama hiyo na kuwa Sh. milioni moja kama dhamana kwa kila mlalamikiwa.

Sababu zilizotolewa na wakili huyo ni kwamba, Kafulila hakuwa na uwezo wa kulipa Sh. 15 milioni zilizotajwa awali kwa mujibu wa sheria ya kesi za uchaguzi.

Baada ya uamuzi huo kutolewa jana mahakamani hapo, Kafulila amesema ameridhika na uamuzi huo wa mahakama na amelipa kiasi hicho cha fedha ili kesi yake ya msingi iweze kusikilizwa na kutolewa hukumu.

Kafulila amesema, kwa mujibu wa jaji washitakiwa watajibu madai hayo ndani ya siku 21 ambapo kesi hiyo inatarajiwa kuanza kusikilizwa mfulizo kuanzia januari mwakani na kwamba, itasikilizwa ndani ya siku 90 na kutolewa hukumu.

“Jaji akitoa hukumu na nisiporidhishwa, nitakata rufaa na kuipeleka mahakama za juu japo sitarajii hayo kutokea. Ninaimani uamuzi wa mahakama utakuwa wa haki kwani nina uhakika wa kushinda kesi yangu,” amesema Kafulila.

By KigomaLive Posted in Habari

Afariki baada ya kula mchanga wa kaburi


KENYA: Binti mmoja amefariki dunia baada ya kula mchanga wa kaburi.

Mhubiri alimshauri ale mchanga huo kwa madai kuwa ana mizimu.

Inasemekana baada ya kunyweshwa dawa, ndivyo hali ya afya ya msichana huyo ilivyozidi kuwa mbaya hadi akapoteza fahamu.

Hata hivyo mhubiri mwenyewe amejitetea akisema huenda ilitokana na familia ya marehemu kutokuwa na Imani na maombi yake ya uponyaji. 

Imenukuliwa kutoka mtandao wa Udaku Special.

Continue reading

By KigomaLive Posted in Habari